Kusimamia Mali za Bwana Hata Ajapo
Januari | Februari | Machi 2023
Somo La 12
Machi 18 - Machi 24
Thawabu za Uaminifu
Thawabu:
Thawabu Yake.
Ni akina nani watapokea thawabu zao kutoka kwa Yesu atakapokuja?
watakatifu (Za. 58:11)
Waliopanda haki (Mit. 11:18)
Waliouawa kwa sababu ya imani zao (Mt. 5:12)
Wale wanaowapenda maadui zao (Lk. 6:35)
Wale wenye ujasiri (Eb. 10:35)
Wale wanaomtafuta (Eb. 11:6)
Manabii, watakatifu, walichao Jina Lake (Uf. 11:18)
Thawabu itakuwa sawa na matendo ya kila mtu (1Kor. 3:8). Je, hiyo inamanisha tunaokolewa kwa matendo yetu? Hapana kabisa!
Wokovu ni karama ambayo kila mmoja anaweza kuipata bila kujali matendo yake (Tit. 3:5). Woye waliokombolewa watapokea “taji” zao, thawabu ya haki (2Tim. 4:8).
Uzima wa milele.
Ni nini hasa tunachostahili? “Ujira” wetu ni nini? Kifo tu. Ni nini Mungu anachotupatia kama “karama”? Uzima wa milele (Rum. 6:23).
Hii ni thawabu tusiyostahili, hatima tofauti kabisa na ile tuliyostaili. Kila mmoja anaweza kuipokea kama ataipokea kwa imani (Yn. 3:16).
Kuwa na Yesu.
Tuna tumaini kama hilo: kuishi katika Yerusalemu Mpya, mji kwa ajili ya “mataifa ya wale waliokombolewa” (Uf. 21:24). Tutapata nini hapo?
Mkono wa Mungu wa upendo utatufuta machozi yetu. Maumivu na kifo havitakuwepo tena (Uf. 21:4)
Bustani ya Edeni, ambapo tutafika na kula kwenye mti wa uzima (Mwz. 3:22; Uf. 22:2)
Yesu. Tutamwona uso kwa uso (Uf. 22:4)
Uaminifu:
Kusimamia kwa ajili ya Bwana…
Mfano wa talanta unashughulika na namna tunavyosimamia kile Mungu alichotupatia, katika muktadha wa Wakati wa Mwisho (Mt. 25:14-30).
Inatupasa kusimamia talanta zetu za asili, karama ambazo Roho Mtakatifu ametupatia, na kila kitu ambacho Mungu ametupatia. Anatupatia kwa kadri tunavyosimamia.
Kila mmoja anawajibika kwa karama na raslimali walizopewa, haijalishi ni ngapi. Thawabu ni ya thamani (Mt. 25:23).
…hadi Ajapo.
Inavyoonekana, Paulo hakuishi maisha ya mafanikio (1 Wakorintho 11:23-28). Na hatujaahidiwa maisha mazuri (2 Tim 3:12)
Hata hivyo, Biblia inasemaje kuhusu kuishi maisha ya furaha na mafanikio (1Tim. 6:6-12)?
Siyo kuwa na mali nyingi
Ni kupata kitu wakati unakihitaji
Ni kung’ang’ania ahadi za Mungu
Ni kumshukuru na kumtumainia Mungu
Pale Yesu atakaporudi, tutapokea thawabu yetu kwa kusimamia kilicho Chake (2Tim. 4:6-8).